Header Ads

TEXAS BAR AND NIGHT CLUB NDIO MPANGO MZIMA KWA MAPUMZIKO YA WEEKEND



WATOTO wa Mujini wanapotumia usemi wa twende zetu tukajivinjari  kijiwe kipya hawakosei kwani hakika huo ndio ukweli wenyewe.

Leo hii naungana na watoto hao wa mujini kwa kuwaambia wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake hasa wa Goba kuwa kwa mahitaji ya kupumzika weekend waende Texas Bar and Night Club ambayo imefanyiwa maboresho makubwa iliyopo Goba Center mita 50 kutoka makutano ya barabara ya kutoka Makongo na barabara kuu ya kwenda Mbezi njia ya kwenda Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ambapo huduma zote za vyakula zinapatikana.

Meneja wa Bar hiyo Tito Justine alitaja huduma zinazopatikana katika Bar hiyo kuwa ni chakula cha aina zote, zikiwepo aina zote za nyama choma inayookwa na wachomaji wenye uzoefu mkubwa.

Alitaja mahitaji mengine kuwa ni vinywaji vya kila aina ikiwepo  juisi halisi iliyotengenezwa kwa viwango vya hali ya juu ambayo inapatikana ndani ya dakika mbili baada ya mteja kutoa oda.

Alitaja huduma zingine kuwa ni ya Cassino, Car Wash, Live Band inayoporomoshwa na Bendi ya Mwenge Jazz kila Jumamosi huku kukiwa na nafasi kubwa ya kuegesha magari na kuwa na ulinzi wa kutosha.

Alisema kwa walaji wa mbuzi katoliki ‘Kitimoto’ pia kinapatikana katika eneo maalumu lilitengwe katika bar hiyo na kufanya kila mtu kufurahia weekend yake akiwa katika bar hiyo yenye mandhari na rafiki kwa mapumziko.

Kivutio kikubwa cha bar hiyo na Night Club ni huduma mbalimbali zinazotolewa na wahudumu warembo na wa  viwango vya juu kama wale wa hoteli za Nyota Tano huku wakiwa nadhifu na wanaotumia lugha nzuri kwa wateja.

Baadhi ya wateja wameupongeza uongozi wa bar hiyo kwa kuja na maono ya biashara hiyo ambayo imewasogezea huduma za chakula na mahitaji mengine.

Muonekano wa Texas Canivo.
Vinywaji mbalimbali vikiwa tayari kwa mauzo.
Mtaalamu akiandaa nyama choma katika bar hiyo.
Matunda yakiwa tayari kwa ajili ya kutengeneza juisi.




 

No comments