Header Ads

SIMULIZI YA MWANAHARAKATI PATRICK GEORGE MITRI

Awasaka viongozi wa Kitaifa kwa miaka 13 awape waraka bila mafanikio

Mwanaharakati Patrick George Mitri

........................

Naitwa Patrick George Mitri (55) nimezaliwa Februari, 1970 Kijiji cha Mgila Kata ya Kwashemshi Wilaya ya Korogwe Vijijini Mkoa wa Tanga.

Mimi ni Mwanaharakati wa Vita dhidi ya Umasikini.

Kabla ya kujigundua mimi ni nani nimepitia katika mapito mengi magumu yaliyopelekea kugundua kilichopo ndani yangu ni nini na hatimaye nikajiita mwanaharakati wa vita hivyo.

Ilikuwa mwaka 2003 nilipo jitambua.

Misukumo iliyokuwa ndani yangu iliongezeka sana baada ya kujitambua nini nani ndani yangu, misukumo yote ililenga wajibu mkubwa wa kitaifa sikujua la kufanya kwani yote yaliyondani yangu niliona mzigo mzito ambao sikujua pa kuutua, wala sikujua nitaanzia wapi na nitamalizia wapi.

“ Dhamira yangu ilinitisha nakuwaza sina elimu kubwa ya kunipa heshima ya kusikilizwa, sina fedha za kunipa thamani ya kusikilizwa wala sina umaarufu wowote wa kunipa kujiamini niliishi kwa mateso na wimbi la mawazo,” alisema Mitri.

Nilikaa kimya na misukumo ya kitaifa iliyo ndani mwangu tangu mwaka 2003 mpaka 2014 ambapo nilipata msukumo wa kuandika waraka kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vyote vya kisiasa nchini.

Bali nihisi ugumu sababu tangu nizaliwe sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa je nikieleza ya siasa nitaeleweka? Kwa maswali niliojiuliza msukumo ulinilazimisha niandike hatimaye mwaka huo 2014 niliandika waraka huo kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vya kisiasa bali nilishindwa kuwapata viongozi hao na kuwakabidhi waraka huo kwani niliamini kwa kuwakabidhi mikononi mwao ana kwa ana ukawa wajibu wangu wa kwanza kuutekeleza.

Simulizi ya kwabza, itaendelea tena kesho kwa maoni piga namba 0717356133. 

No comments