Header Ads

BALOZI DKT. NCHIMBI: CCM KUENDELEA KUMUENZI HAYATI MKAPA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin Mkapa alipozuru katika Kijiji cha Lupaso, Masasi.

..........................

Na Mwandishi Wetu, Mtwara 

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Balozi Dkt Emmanuel Nchimbi ametembelea kaburi la aliyekuwa Rais wa Awamu ya 3 , Hayati Benjamin William Mkapa katika Kijiji cha Lupaso Mkoani Mtwara .Dkt Nchimbi ametembelea kaburi hilo Julai 28, 2024. na kutoa Pole kwa familia na kuzungumza na Wananchi wa Lupaso.

Balozi Nchimbi amesema "naomba nikiri kuwa Mimi ni mwanafunzi wa hayati na nimekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Taifa katika kipindi Chake kwani ndio alinilipia Ada ya kusoma Chuo kikuu na alikuwa mfuatiliaji sana na alitulea na sio Sisi lakini kwa Watanzania wote aliwalea pia alikuwa mzalendo kwa Nchi alifanya mabadiliko Makubwa kwa Nchi yake na Kwa Chama Chake lakini yote CCM chini ya Dkt Samia tutaendelea kuyaenzi Yale yote aliyoyoacha Hayati Benjamin Mkapa na pamoja hayo nimeambiwa kero za hapa na tumezichukua lakini CCM inatoa Shilingi Milioni 10 kuanza kukarabati Shule ya hapa Lupaso".

Katika ziara hii Dk Nchimbi ameambatana na Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amosi Makalla, Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) pamoja na Katibu wa NEC- Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Rabia Abdallah Hamid.Katibu wa NEC-Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Amosi Makalla akiweka shada la maua.Katibu wa NEC-Organaizesheni Ndg. Issa Ussi Haji (Gavu) akiweka shada. Katibu wa NEC- Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg. Rabia Abdallah Hamid akishiriki kuweka shada la maua katika kaburi hilo.

Heshima ikitolewa mbele ya jeneza la Hayati Benjamin Mkapa.
Dkt. Nchimbi akizungumza na wananchi alipozuru kaburi hilo.

No comments