PROMOSHENI YA BIA YA WINDHOEK KUTIKISA TEXAS BAR NA NIGHT CLUB GOBA JIJINI DAR ES SALAAM
Muuonekano wa Bia aina ya Windhoek
...................................
Na Dotto Mwaibale.
LEO katika kiota cha
maraha Texas Bar na Night Club iliyopo Goba jijini Dar es Salaam kuanzia saa 8
mchana huu kutakuwa na Prosheni kubwa ya aina yake ya vinywaji mbalimbali vya
kisasa vinavyosambazwa hapa nchini na Kampuni ya Heineken Beverages ambayo ni maarufu duniani kwa
uuzaji wa vinywaji.
Moja ya kinywaji kitakachokuwepo kwenye promosheni hiyo
ni Bia aina ya Windhoek ambayo ni ya hali ya juu inayotengenezwa nchini Namibia ikiwa na ladha nyororo,
ya kuburudisha, inayoheshimika kuwa ni bia bora zaidi, na iliyo na ubora kamili inayopatikana kila kona ya Tanzania kwa bei nafuu na kupendwa na idadi kubwa ya watanzania.
Moja ya sifa kubwa ya bia
hiyo ni kutokuwa na ‘eng’iova’ kwa mnywaji ambae akiamka asubuhi anajisikia
vizuri na kumfanya aendelee na shughuli zake akiwa na furaha.
Afisa mmoja wa kampuni
hiyo ya Heineken Beverages ambaye hakupenda jina lake liandikwe akizungumzia
promosheni hiyo alisema itaanza saa nane mchana wa leo Mei 24, 2025 na
itaendelea hadi saa sita usiku na kuwa kesho itafanyika tena katika eneo hilo
la Goba na kueleza kuwa itakuwa endelevu.
Alisema promosheni hizo
zimelenga kutangaza vinywaji hivyo pendwa ambavyo vikinunuliwa kwa wingi
vitachangia ukuaji wa uchumi wa nchi.
Aidha ametoa wito kwa
wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake hasa vya Goba kufika Texas Bar na Night
Club kushiriki promosheni hiyo.
Kwa upande wake Meneja wa
Bar hiyo Tito Justine amesema wadau mbalimbali watakaofika kwenye promosheni
hiyo wafike kwa wingi kufurahi huduma zilizopo kama ya vyakula vya aina
mbalimbali vilivyoandaliwa na wapishi wa viwango vya juu.
Alitaja
huduma zingine ambazo zipo kwenye bar hiyo kuwa ni ya Cassino, Car Wash, Live
Band inayoporomoshwa na Bendi ya Mwenge Jazz kila Jumamosi huku kukiwa na
nafasi kubwa ya kuegesha magari na kuwa na ulinzi wa kutosha.
Alisema katika bar hiyo
kuna hali nzuri ya usalama hivyo aliwaomba wadau hao kufika kwa wingi kushiriki
promosheni hiyo.
Muonekano wa Kiota cha maraha Texas Bar and Night Club iliyopo Goba jijini Dar es Salaa.



Post a Comment