Header Ads

PROMOSHENI ZA WINDHOEK, TEXAS BAR AND NIGHT CLUB GOBA JIJINI DAR ES SALAAM ZANOGESHA BAR HIYO

Muonekano wa bia aina ya Windhoek.
..............................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

PROMOSHENI ya bia ya Windhoek inayoendelea kufanyika eneo la maraha yaani Texas Bar na Night Club iliyopo Goba jijini Dar es Salaam zimeinogesha bar hiyo na kuwa kimbilio la watu wengi kwenda kupumzika na kujipatia vinywaji vya kisasa vinavyosambazwa nchini na Kampuni ya Heineken Beverages ambayo ni maarufu si kwa Tanzania pekee bali duniani kote kwa uuzaji wa vinywaji.

Leo tena katika bar hiyo ya maraha kuanzia saa 8 mchana huu kutakuwa na Promosheni kubwa ya aina yake ya vinywaji mbalimbali vya kisasa ikiwemo bia ya Windhoek ambayo imekuwa ikichangamkiwa na wanywaji kutokana na ubora wake wa kimataifa.

Bia hiyo ya Windhoek Lager ambayo ina ubora wa hali ya juu inatengenezwa nchini Namibia na kutokana na ubora wake imeenea duniani kote.

Kinywaji hicho kina ladha nyororo, ya kuburudisha, inayoheshimika kwa ubora zaidi ambacho hapa nchini kinapatikana kila kona kwa bei nafuu na kupendwa na idadi kubwa ya watanzania.

Moja ya sifa kubwa ya bia hiyo ambayo imejizolea umaarufu ni kutokuwa na ‘eng’iova’ kwa mnywaji ambae akiamka asubuhi baada ya kuinywa anajisikia vizuri na kumfanya aendelee na shughuli zake akiwa na furaha.

Afisa mauzo wa kampuni hiyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe alisema promosheni hizo zimelenga kutangaza vinywaji hivyo pendwa ambavyo vikinunuliwa kwa wingi vitachangia ukuaji wa uchumi wa nchi.

“ Bei ya bia hii ya Windhoek katika promosheni yetu ni ya chini kabisa kwani katoni moja yenye bia sita ambayo kwa kawaida inauzwa Sh. 24,000 kwa bei ya promosheni tunauza Sh.20,000 yaani ni bei rafiki kabisa kwa wanywaji,” alisema Afisa huyo.

Aidha ametoa wito kwa wakazi wa Dar es Salaam na vitongoji vyake hasa vya Goba kufika Texas Bar na Night Club kushiriki promosheni hiyo. 

Meneja wa Bar hiyo Tito Justine amesema promosheni zinazoendelea za bia hiyo zimechochea ongezeko la wadau wanaofika kwenye bar hiyo kwa wingi na kufurahiya huduma zilizopo kama ya vyakula vya aina mbalimbali na nyama choma za aina zote vinavyoandaliwa na wapishi wenye uzoefu wa viwango vya hoteli ya nyota tano.

Alitaja huduma zingine ambazo zipo kwenye bar hiyo kuwa ni ya Cassino, Car Wash, Live Band inayoporomoshwa na Bendi ya Mwenge Jazz kila Jumamosi huku kukiwa na nafasi kubwa ya kuegesha magari na kuwa na ulinzi wa kutosha.

Alisema kwa walaji wa mbuzi katoliki ‘Kitimoto’ pia kinapatikana katika eneo maalumu lilitengwe katika bar hiyo na kufanya kila mtu kufurahia weekend yake akiwa katika bar hiyo yenye mandhari na rafiki kwa mapumziko.

Baadhi ya wateja wameupongeza uongozi wa bar hiyo kwa ushikiano mkubwa na kampuni hiyo na kufanya promosheni ya vinywaji vyao wakati wowote na wafurahiye mapumziko yao ya mwishoni mwa wiki.

Muonekana wa Texas Bar and Night Club iliyopo Goba jirani na mzunguko wa magari barabara ya kutoka Makongo na ile ya kwenda Mbezi.

Nyama choma ikiandaliwa kwa ajili ya wateja wa bar hiyo.

 Hiki ndio Texas Bar and Night Club kiota cha maraha kilichopo Goba.
......................................................................................................................

Kwa mtu yeyote atakayependa kufika katika bar hiyo pendwa na kufurahia huduma zao nzuri kwa maelezo zaidi anaweza kuwasiliana kwa wahusika kwa namba (0714219701)

No comments