SIMULIZI YA MWANAHARAKATI PATRICK GEORGE MITRI
Awasaka viongozi wa Kitaifa kwa miaka 13 awape waraka bila mafanikio
Patrick George Mitri
.........................
Misukumo ya
kitaifa ilinizidi kila wakati nilipokata tamaa na kuona kilichondani yangu ni
kigumu kwangu na ndipo nilipoomba ushauri kwa watu wa karibu yangu wenye upeo
ulionizidi, ushauri wao uliangukia neon moja nianzishe Shirika lisilo la
Kiserikali (NG’Os) ndiyo nitaweza kuionesha jamii kipaji changu na kuwatumikia.
Sikuchelewa
niliingia kwenye wajibu wa kutafuta watu niwape wazo langu ambapo ulitokea
ugumu na msukumo ulinielekeza nipate watu ambao hawajawai kujiunga na vyama vya
siasa toka wazaliwe kama mimi, wawe ndio waanzilishi wa shirika hilo (ASASI).
Nilifanikiwa
kuwapata licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa ambapo niliwashauri na kunielewa.
Baada ya
hapo tulikuwa na majukumu matatu ambayo ni kama ifuatavyo:
1.Kuunda kikundi cha Vita dhidi ya
umasikini.
2.Kutengeneza katiba
3.Kusajili shirika la vita dhidi ya
umasikini kitaifa.
Tulifanikiwa kwa kiwango kikubwa ikapatikana katiba ambayo ilipitishwa
kwa mujibu wa sharia na kuipeka Wizara ya Mambo ya Ndani Jijini Dar es Salaam.
Kwa bahati mbaya nilipofika mapokezi na kupokelewa katiba ili nipate
maelezo wafanyakazi wa kitengo cha mapokezi walipata taarifa ya msiba wa
mfanyakazi mwenzao ambaye alikuwa ni mwanamke tukio hilo kwao lilikuwa la
ghafla kwani niliona hadi wanaume wakitoka machozi ambapo sikupata maelezo
yoyote zaidi ya kukabidhi katiba na kuacha namba yangu ya simu kwa taarifa
zaidi.
Baada ya hapo nilitafuta usafiri na kurudi nyumbani Korogwe nikiwa
nimechoka na kukata tamaa.
NAMBA 3
Niliporudi nyumbani ninakoishi Kijiji cha Mgila Korogwe Vijijini, usiku
nilipata msukumo ulionionesha ninafanya kosa kubwa kitaifa kwa wakati ule
kufuatilia usajili wa Shirika.
Niliona nguzo tatu ambazo ni Muhimiri wa Taifa na zile nguzo niliziona
zilivyo ambazo ni kama ifuatavyo:
1.Dini
2.Siasa
3. Ulinzi na Usalama.
Usiku ule kunakitu nilichokibaini ambacho ni jambo kubwa la kitaifa kama
hili la vita dhidi ya umasikini lina shabaha kubwa ni lazima lipite kwa makundi
hayo matatu na kueleweka kwao mwanzo na mwisho wake walichakate, walichuje na
hatimaye wawe na jibu moja kama linafaa kitaifa ndipo lifuate utaratibu wa
kisheria wa kuanzishwa Shirika hilo la kitaifa na kama halifai lisuruhusiwe
kuanzishwa kwa maslahi ya taifa.
Kwa sababu waliondani ya usimamizi wa mihiri hiyo mitatu ya taifa ndiyo
wanaobeba lawama taifa likiyumba na pia ubeba heshima na sifa njema taifa
liking’aa.
Niliona wajibu wao wa haki kuchuja kwa pamoja masuala makuu ya kitaifa kabla hayajafika ngazi ya mujibu wa sheria kwa kuanzishwa mashirika ya kiraia ndiyo ikawa mwisho wa wazo la kuanzisha shirika hilo nisijue la kufanya huku msongo wa mawazo ukitamalaki na kukata tamaa.
Simulizi ya pili, itaendelea tena kesho kwa maoni piga namba 0717356133.




Post a Comment