REGINA NDEGE MBUNGE MWENYE UPENDO ANAYEGUSA MAISHA YA WATU MANYARA
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Manyara na Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe. Regina Ndege, akimjulia hali Mama Mzazi wa Mjumbe wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Manyara, Inyasi Mpaki na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Wilaya ya Babati Vijijini, Solomon Mpaki ambaye amelazwa Hospitaaali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma anasumbuliwa na nyonga.
...........................
UPENDO ni hali ya moyo wa mtu kuwa na hisia kali ya kujali, kuhurumia kuwa na uchungu dhidi ya mtu mwingine bila ya kinyongo.
Ni sifa ya
thamani inayohusisha ustahimilivu na
kutafuta mema kwa wengine kama biblia inayoeleza upendo kama amri kuu,
ikimaanisha ni msingi wa maisha ya kiroho.
Mbunge wa
Viti Maalumu Mkoa wa Manyara na Naibu Waziri
wa nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe.
Regina Ndege ni kiongozi mwenye upendo ambaye anagusa maisha ya watu.
Wananchi wa
Mkoa wa Manyara wanamuita Mama wa Faraja wa mkoa ho.
Mhe. Ndege
wakati wote amekuwa mstari wa mbele kushirikiana na wananchi katika mambo
mbalimbali ya maendeleo, furaha na huzuni.
Jambo hilo
limekuwa likimuweka jirani zaidi na wananchi na kufanya apendwe.
Mhe. Ndege
kutokana na hulka yake ya kuwa na wananchi karibu amekuwa akiweka kipaumbele
hasa wanapokuwa na changamoto mbalimbali zikiwepo za ugonjwa.
Kiongozi
huyu amekuwa hapoi katika shughuli mbalimbali zinazowahusu wananchi ambapo leo alikwenda Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini
Dodoma kumjulia hali Mama Mzazi wa Mjumbe
wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Manyara, Inyasi Mpaki na Mwenyekiti
wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Wilaya ya Babati Vijijini, Solomon Mpaki
ambaye anasumbuliwa na nyonga.
“Maisha ya Mhe. Ndege yamekuwa kielelezo kwa
wana Manyara na Taifa kwa ujumla hasa katika masuala ya siasa na kijamii,”
alisema Kulwa Mkamba.
Mkamba alisema mambo anayofanya Mhe. Ndege yamekuwa ni darasa kwa watu mbalimbali siyo tu wa Mkoa wa Manyara bali Tanzania kwa ujumla.
Mhe. Regina Ndege, akimjulia hali Mama huyo. Wengine ni Wajumbe wa Baraza la Wazazi kutoka Mkoa wa Manyara. Mhe. Regina Ndege, akimjulia hali Mama huyo. Kulia ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Wilaya ya Babati Vijijini, Solomon Mpaki......................................
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990.






Post a Comment