Header Ads

CCM KIGOMA YAFANYA UTEUZI WAGOMBEA NAFASI YA UDIWANI, UCHAGUZI KUFANYIKA JUNI MOSI , 2026

Katibu wa Siasa, Uenezi na Mafunzo wa CCM Mkoa wa Kigoma Deogratius Nsokolo, akizungumzia kuhusu uteuzi wa wagombea wa nafasi za udiwani katika Kata za Nyamgali wilayani Buhigwe na Nyumbigwa wilayani Kasulu katika kikao kilicho keti Aprili 30, 2026.

....................................

Na Mwandishi Wetu, Kigoma

Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa kigoma imefanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za udiwani katika uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata za Nyamgali wilayani Buhigwe na Nyumbigwa wilayani Kasulu.

Katibu wa siasa, uenezi na mafunzo wa CCM Mkoa wa kigoma Deogratius Nsokolo amesema, Katika kikao hicho ambacho kimeongozwa na mwenyekiti wa CCM Mkoa Jamal Tamim kimemteua Ludovick Nyaruguru Boyi kugombea katila kata ya Nyumbigwa wilayani Kasulu na Anania Jest Mbango  kuwania udiwani katika kata ya Nyamgali wilayani Buhigwe.

Uchaguzi katika kata hizo utafanyika Juni Mosi mwaka huu na unafanyika kufuatia vifo vya madiwani wa kata hizo .

Halmashauri kuu ya CCM Mkoa pia imeweka mikakati kadhaa ya kuimarisha Chama.

Viongozi wa CCM Mkoa wa Kigoma wakiwa kwenye kikao hicho cha uteuzi. Katikati ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma Comred Jamal Tamim, kushoto kwake ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa Abdulkadri Mushi na kulia kwake ni Katibu wa CCM waMkoa huo, Christopher Palangyo.

 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoaa wa Kigoma wakiwa kwenye kikao hicho.

No comments